KLABU ya waandishi wa habari Mkoa wa Morogoro (Morogoro Press Club) mchakato wa kuanzishwa mwaka 1996 ilipofika tarehe 13/3/1997 ikapata usajili Wizara ya Mambo ya ndani na kupata cheti cha usajili chenye namba. SO.NO.9009 ikiwa na wanachama 20 kwa sasa Morogoro Press Club ina wanachama 80.
Ofisi ya MOROPC ipo katika jengo la Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Kata ya Kingo mkabala ya Mahakama ya mwanzo ya Nunge,Manispaa ya Morogoro.
VIONGOZI WA MOROGORO PRESS CLUB 2015-2018
Nickson Mkilanya-Mwenyekiti
Ashhton Balaigwa-Makamu Mw/kiti
Jonh Kidasi Katibu Mtendaji
Jimmy Mengele-Katibu Msaidizi
Agness Haule - Mweka hazina msaidizi
Severin Blasio-Mjumbe
Christina Haule - Mjumbe
Fadhil Rashid-Mjumbe
Thadei Hafigwa-Mratibu
1. Ni chama cha kitaaluma malengo yake mahususi ni kujenga mahusiano miongoni mwa wanachama na makundi yenye makusudio tofauti ikiwa ni pamoja na taasisi za raia.
2. Kuwa kitovu cha masuala ya waandishi wa habari katika mkoa wa Morogoro.
3. Kuhakikisha kuwa wanachama wake wanafanyakazi kulingana na maadili ya waandishi wa habari kama ilivyofafanuliwa na Baraza la Habari.
4. Kuinua kiwango cha taaluma katika tasnia ya habari kwa kuendesha mafunzo mafupi mafupi kwa wanachama wake.
5. Kuwezesha wanachama kutumia rasilimali chache zilizopo katika kuboresha shughuli za ukusanyaji na usambazaji wa habari miongoni mwa waandishi wa Watanzania.
6. Kuimarisha ushirikiano miongoni mwa waandishi wa habari,watoa habari na taasisi za kitaaluma zenye kulenga kuongeza ufanisi katika habari na mawasiliano kwa maanufaa ya wanachama wote na jamii na kuitangaza vema Mkoa wa Morogoro ili kusukuma maendeleo ya wananchi kwa kasi.
7. Kuwalinda waandishi wa habari dhidi ya madai yenye mwelekeo wa kitaaluma.
DHAMIRA:"Kuwaimarisha waandishi wa habari Kitaaluma"
DIRA:"Kuwa na jamii yenye uhuru wa kujieleza na Uhuru wa Habari"
Morogoro Press Club kama ilivyo Taasisi nyingine mara baada ya kupata usajili wake ilipita katika hatua mbalimbali za uongozi.
Awamu ya kwanza 1997-2000
Ndg.Anaclet Rwegayura-Mwenyekiti
Bi.Halima Kihemba -Makamu Mwenyekiti
Ndg.Wilson Karuwesa- Katibu na mtunza fedha.
Wajumbe watatu wa kamati tendaji
Ndg.Richard Mwangulube
Ndg.Said Mtaalamu
Ndg.Aziza Msuya.
Awamu ya pili 2001 hadi 2002
Ndg Said Dogori Mwenyekiti
Ndg.Bonventure Mtalimbo-Makamu Mwenyekiti
Marehemu Aidan Libenanga-Katibu Mkuu
Bi.Monica Lyampawe- Mtunza fedha.
Wajumbe watatu wa kamati tendaji
Ndg.Simon Berege
Ndg.Halfan Diyu
Ndg.Richard Mwangulube.
Awamu ya tatu 2002 hadi 2004.
Marehemu Seraph Kuandika-Mwenyekiti
Ndg.Bujaga Kadago- Makamu Mwenyekiti
Ndg.Sita Peter wake-Katibu Mkuu
Bi.Merina Robert- katibu Mkuu msadizi.
Bi.Kasilda Mgeni- Mtunza fedha.
Wajumbe watatu wa kamati ya tendaji
Ndg.Nikson Mkilanya
Ndg.Samweli Msuya
Ndg.James Mkisi.
Awamu ya nne Julai 2004 hadi 2007.
Ndg.Bonventure Mtalimbo- Mwenyekiti
Bi.Idda Mushi- Makamu Mw/kiti.
Ndg.Thadei Hafigwa- Katibu Mkuu
Ndg.Said Mtaalam katibu mkuu msaidizi
Ndg.Samweli Msuya- Mtunza fedha
Wajumbe watatu wa kamati tendaji
Marehemu Gilbert Suleman
Ndg.Said Dogoli
.Ndg.Wilson Karuwesa
.
Awamu ya tano Julai 2007 hadi 2011
Ndg.Bonventure Mtalimbo- Mwenyekiti
Bi. Idda Mushi- makamu Mw/kiti
Ndg.Thadei Hafigwa -Katibu Mkuu.
Bi.Devota Minja K/Msaidizi
Ndg.Samweli Msuya- Mtunza fedha
Wajumbe watatu wa kamati tendaji
Ndg.Ramadhani Libenaga
Ndg.Ashton Balaigwa
Bi. Lilian Lucas
Awamu ya sita Novemba 2011-2014
Ndg.Aziz Msuya-Mwenyekiti
Bi.Devota Minja-Makamu Mw/kiti
Ndg.Abedi Dogoli-Katibu Mtendaji
Bi.Lilian Lucas-Mwekahazina
Wajumbe watatu wa kamati tendaji
Bi.Latifa Ganzel
Bi.Monica Liampawe
Ndg.Venance George
Mabadiliko ya kimfumo
Mwaka 2011 Umoja wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania ambapo sisi ni miongoni mwa wanachama wake ulinda mfumo wa kuwa na waratibu wa Klabu katika mikoa yote wanaoajiliwa ili kuhakikisha ya kuwa shughuli zote za kiutendaji vinafanyika. Kwa mkoa wetu wa Morogoro nafasi hiyo inashirikiwa na Ndg.Thadei Hafigwa
Mabadiliko ya kimifumo Awamu Saba Machi 2013-Agosti 2015
Bi.Idda Mushi-Mwenyekiti
Ndg Nickson Mkilanya-Makamu Mw/kiti
Ndg.Abedi Dogoli-Katibu Mtendaji
Ndg.Ramadhan Libenanga-Katibu msaidizi
Bi.Lilian Lucas-Mwekahazina
Ndg.Peter Kimath-Mwekahazina Msaidizi
Wajumbe watatu wa kamati tendaji
Ndg.Ashton Balaigwa
Ndg.Fadhil Rashid
Bi.Vaileth Mbwillo
Ndg.Thadei Hafigwa-Mratibu
Awamu ya Nane Agosti 2015-Agosti 2018
Ndg.Nickson Mkilanya-Mwenyekiti
Ndg.Ashton Balaigwa-Makamu Mw/kiti
Ndg.John Kidasi-Katibu mtendaji
Ndg.Jimmy Mengele-Katibu Msaidizi
Bi.Merina Robert-Mwekahazina
Bi.Agnes Haule-Mwekahazina Msaidizi
Wajumbe watatu wa Kamati tendaji
Ndg.Fadhil Rashid
Ndg.Severin Blasio
Bi.Christina Haule
KAMATI YA MAADILI MOROGORO PRESS CLUB
Jukumu la kamati hii ni kuhakikisha ya kuwa inasimamia masuala yote ya kitaaluma na kusuluhisha malalamiko kati ya waandishi wa habari na wadau pale inapojitokeza upande mmoja kuona haikutendewa haki
Viongozi wa kamati hii ni÷
Mzee Rashid Lusewa-Mwenyekiti kamati ya maadili
Ndg.Saidi Dogoli-Mjumbe
Ndg. Bonventure Mtalimbo-Mjumbe
Ndg.Wilson Karuwesa
Sheikh Ally Omar-Mjumbe
Rev.Fr.Makseyo-Mjumbe
Ndg.John Nyabinyiri-Mwanasheria
Bi.Aziza Msuya-Mjumbe
Ndg.Nickson Mkilanya-Mjumbe
Ndg.John Kidasi-Mjumbe
Ndg.Thadei Hafigwa-Mjumbe
Pia Morogoro Press Club ina kamati ndogondogo za kusaidia kuharakisha utekelezaji wa majukumu ya kila siku.
Kamati ya mipango uchumi, fedha na Mahusiano
Majukumu ya kamati hii ni kushirikiana na Kamati tendaji katika kutafuta vyanzo mbalimbali vya mapato ili kuhakikisha ya kuwa Klabu inapata mapato
Viongozi wa kamati hii ni
Kasilda Mgeni-Mwenyekiti
Latifa Ganzel-Katibu
Merina Robert-Mwekahazina
Kamati ya ujenzi na ustawi wa Jamii.
Majukumu ya kamati hii ni kushirikiana na Kamati tendaji katika kutafuta mfumo wenye tija katika kuhakikisha ya kuwa Klabu inakuwa na jengo la kitega uchumi.
Pia kuhakikisha ustawi wa wanachama na jamii unaimarika hasa kwenye sherehe,ugonjwa na vifo kwa kuandaa mfumo maalum utakaosaidia malengo yaliokusudiwa yanafikiwa.
Viongozi wa kamati hii ni
Monica Liampawe-Mwenyekiti
Lilian Lucas-Katibu
Agnes Haule-Mwekahazina.
Mkoa wa Morogoro una waandishi zaidi ya 100 ambao wanajumuisha wanachama wa Morogoro Press Club,na wasio wanachama ambao wanaofanyakazi katika vyombo mbalimbali vya habari vya serikali na binafsi.
Mlezi wetu wa Morogoro Press Club ni Mkuu wa Mkoa Mstaafu,Mhe.Stephen Joshua Mashishanga
MAFANIKIO YA MOROPC
Miongoni mwa mafanikio yaliopatikana ni pamoja na
1. Kuweza kupaza sauti kwa wasio na sauti.
2. Kuwa kiungo kati ya serikali na wananchi(people centered)
3. Imeweza kujiunga na taasisi za kitaaluma kama vile Umoja wa Klabu za waandishi wa habari Tanzania (UTPC) na Baraza la Habari Tanzania(MCT).
4. Kutokana na kuwa mwanachama wa taasisi hizo MOROPC kimenufaika vitendea kazi(vifaa vya ofisi na samani) kama kompyuta, TV, Printer,scanner,kamera ya picha za mnato na picha za video(moving)
5. Pia wanachama wanapata mafunzo na semina za kitaaluma katika kukumbusha masuala yote ya kimaadili.wanachama wanapata machapisho mbalimbali ya kitaaluma.
6. Kuwa na blog yenye lengo la kuwahabarisha jamii kazi na majukumu mbalimbali ya taaluma ya habari.
7. Kuanzisha mfumo maalum wa kusaidiana katika masuala mbalimbali ya kijamii(bima ya afya,)
MIKAKATI YA KLABU.
Pamoja na mafanikio yote hayo pia MOROPC ina mikakati ya muda mrefu na muda mfupi,ikiwa ni pamoja na kumiliki jengo lake la kitega uchumi ili kuwa na uandishi wa habari wa kiuchumi.
Morogoro Press Club ipo katika mchakato wa kuanzisha gazeti la Klabu kwa ajili ya kupanua wigo wa kuwahudumia wananchi wa maeneo yote mjini na vijijini ikiwa ni fursa yao kutoa maoni,changamoto na mafanikio wanayoyapata katika shughuli zao za kiuchumi,Kijamii na kiutamaduni.
MAHUSIANO NA TAASISI ZINGINE
MOROPC imekuwa na mahusiano na Taasisi za ndani na nje ya nchi AkibaUhaki foundation iliopo Nchini Kenya,Umoja wa Klabu za waandishi wa Habari Tanzani(UTPC) na Baraza la Habari Tanzania(MCT).
CHANGAMOTO
Morogoro Press Club haina jengo lake la ofisi inategemea zaidi kupanga na wakati mwingine kushindwa kutimiza majukumu yetu ya kuwahudumia wananchi katika kiwango chenye ufanisi.
MOROPC inakabiliana na changamoto ya raslimali fedha kwa ajili ya kutekeleza mipango mkakati ya kuimarisha taasisi na wanachama wake.










Hakuna maoni:
Chapisha Maoni